Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Celtel yakabidhi mil. 57/- kwa washindi
Celtel yakabidhi mil. 57/- kwa washindi
By Habari Tanzania | Published  10/19/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
na Amana Nyembo

KAMPUNI ya simu za mkononi ya Celtel, imekabidhi hundi zenye thamani ya sh milioni 57 kwa washindi 21 wa promosheni ya ‘Jishindie ndoto yako’.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kukabidhi hundi hizo jana katika Hoteli ya Holiday Inn, Meneja Masoko wa kampuni hiyo, Margaret Kositany alisema miongoni wa washindi hao, wanne ni wa hundi ya milioni 10 kwa kila mmoja na washindi 17 ni hundi ya sh milioni moja kila mmoja.

Alisema lengo la Celtel ni kuboresha maisha ya wateja wanaoendelea kupata huduma za mawasiliano na kuwapa fursa zaidi za kuboresha maisha yao.

“Lengo letu Celtel ni kuhakikisha kuwa tunaboresha maisha ya wateja wetu na tunafanya juu chini kuhakikisha kuwa wanaendelea kupata huduma bora za mawasiliano, pia kuwapa fursa za ziada za kuboresha zaidi maisha yao,” alisema Margaret.

Akizungumza baada ya kupokea hundi ya sh milioni 10, Selemani Mohamed Shemndoro (46) ambaye ni mkazi wa Majumba Sita, Ukonga, Dar es Salaam, aliishukuru kampuni hiyo na kuahidi kutumia fedha hizo katika kuendeleza biashara zake na familia.

Washindi wengine wa sh milioni 10 ni Mussa Mbwilo, Yusuf Rajabu na Zahara Abdu.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.