Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Hakuna atakayekufa njaa K’njaro-Dk.Shein
Hakuna atakayekufa njaa K’njaro-Dk.Shein
By Habari Tanzania | Published  05/14/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated

Makamu wa Rais, Dk. Ali Mohammed Shein, amesema kuwa Serikali itahakikisha kwamba hakuna mtu atakayekufa njaa kwenye maeneo yote yaliyokumbwa na mafuriko mkoani Kilimanjaro.

’’Serikali itahakikisha kwamba inatoa kila aina ya msaada kwa wote waliopatwa na janga la mafuriko na kuwasaidia kurejea katika maisha yao ya kawaida,’’ alisema Dk. Shein.

Aliyasema hayo katika mkutano wa hadhara alipozungumza na wakazi wa kijiji cha Mandaka Mnono kitongoji cha Uswahilini, moja ya maeneo yaliyokumbwa na mafuriko.

Mafuriko hayo yalivikumba vijiji 16 vya Moshi ambavyo vipo katika kata nne za Kahe, Old Moshi Magharibi, Kirua Vunjo Kusini na Kahe Mashariki.

Katika ziara hiyo ambayo ilikuwa na lengo la kuwapa pole wananchi walioathirika, Dk. Shein alifuatana na Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge) Bw. Juma Akukweti.

Katika ziara hiyo, Dk. Shein alizunguka kwa helikopta ili kujionea athari ya mafuriko hayo na aliwaambia wananchi hao kuwa amejionea athari hiyo na akawahakikishia kwamba hakuna atakayekufa njaa.

’’Serikali italeta chakula na kitagawiwa bure kwa walioathirika na kwa wale walioharibikiwa nyumba zao jitihada za kuwahifadhi zinafanywa,’’ alisema.

Kwa upande wao wananchi walimwomba Makamu wa Rais kuwajengea shule na zahanati kwa kuwa huduma hiyo hawana hivyo kulazimika kufuata huduma hiyo eneo la mbali.



  • SOURCE: Nipashe

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
This article has been added to your 'Favourites' list.
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.