Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Walemavu wapatiwa baiskeli 550
Walemavu wapatiwa baiskeli 550
By Habari Tanzania | Published  10/18/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
na Peter Kimath, MSJ

SHIRIKA la Free Wheel Chair limetoa msaada wa baiskeli 550 kwa walemavu, zenye thamani ya sh 175,000,000, kupitia Kanisa la Christian Mission lililopo jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Askofu wa kanisa hilo, Mgullu Kilimba, alisema kanisa lao linatambua wajibu wake katika kushirikiana na serikali kuwaondolea Watanzania kero zinazosababishwa na ujinga, umaskini na maradhi.

Mgullu alisema wameandaa fomu maalumu kwa walengwa ambazo mlemavu atajaza na kuthibitishwa na viongozi wa kanisa na serikali za mita kuwa hana baiskeli.

Amewaomba wasamaria wema na serikali kwa ujumla kuchangia zoezi hilo, ili waweze kusambaza mikoani. Zoezi hilo litagharimu sh 15,000,000.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.