Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Mkurugenzi Ilala atakiwa mahakamani
Mkurugenzi Ilala atakiwa mahakamani
By Habari Tanzania | Published  10/18/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
na Irene Mark

MAHAKAMA ya Wilaya ya Ilala, imemtaka Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, John Lubuva, kutoa sababu za kukiuka amri ya mahakama na kuwafukuza wafanyabiashara ndogo ndogo au wamachinga kwenye maeneo yao ya biashara isivyo halali.

Amri ya kuitwa mahakamani mkurugenzi huyo, ilitolewa jana na Hakimu Mkazi Bahati Ndesaruwa, alipokuwa akisikiliza maombi ya wanachama wa jamii ya maendeleo ya kutaka mkurugenzi huyo kufungwa jela au kupewa adhabu kali kwa kukiuka amri ya mahakama na kuwabughudhi wamachinga hao.

Awali, wakili wa mkurugenzi huyo, Mponela, aliiomba mahakama kumpa muda ili mteja wake awasilishe majibu ya hati ya kiapo cha walalamikaji iliyowasilishwa mahakamani hapo Oktoba 2, mwaka huu na wakili wao, Aboubakar Salim wa Kampuni ya uwakili ya Taslima.

Baada ya maombi ya wakili Mponela, upande wa walalamikaji uliomba mahakama kutoa ruhusa ya wamachinga hao kuendelea na biashara zao kwenye maeneo ya awali wakati mahakama inasubiri majibu ya mkurugenzi.

Kabla ya kuahirisha shauri hilo hadi Oktoba 26, mwaka huu litakapotajwa tena, Hakimu Ndesaruwa, alisema mahakama itasubiri kwanza sababu za mkurugenzi kabla ya kuamua ama kuwaruhusu wamachinga au kuendelea na shauri hilo.

Dai la msingi la wamachinga hao ni kutaka kurejeshwa katika maeneo hayo na kutambuliwa kihalali. Pili, wanataka walipwe sh milioni 2.5 kila mmoja kama kifuta jasho kwa ajili ya usumbufu walioupata kutoka kwa mkurugenzi na wafanyakazi wa manispaa ya Ilala.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.