Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Lowassa: Watendaji msikubali kutapeliwa na wawekezaji
Lowassa: Watendaji msikubali kutapeliwa na wawekezaji
By Habari Tanzania | Published  10/11/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Na James Marenga, Tanga

WAZIRI Mkuu, Edward Lowassa, amewataka wananchi wa Tanga kutokubali kutapeliwa na wawekezaji na kuwauzia viwanja kwa bei nafuu.

Alisema hayo jana kwenye mkutano wa hadhara mjini hapa.

Alisema wawekezaji wanaweza kutumia ujanja wa kupata viwanja kwa bei chee. “Wawekezaji hawa wa sekta ya utalii wanaweza kuwarubuni mkauza kiwanja cha sh milioni 20 kwa sh milioni 10,” alisema.

Waziri Mkuu alisema wananachopaswa kufanya ni kuwahusisha maofisa ardhi.

Alisema sekta ya utalii inakua kwa kasi wilayani humo, mwananchi anachotakiwa ni kuchangamkia kwa kuingia nao ubia au kuchangamkia ajira zitakazotokana na sekta hiyo.

Wilaya ya Pangani ni moja ya wilaya zenye historia ya mambo ya kale, ikiwamo biashara ya utumwa. Akiwa wilayani hapo alitoa sh milioni tatu kutunisha mfuko wa vyama vya kuweka na kukopa (SACCOS) za kina mama za Jitegemee, Mshikamano na ya Wakulima, na mke wa Waziri Mkuu, Regina Lowassa, alitoa sh milioni moja


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.