MFANYABIASHARA wa samaki wa eneo la Mafiga mkoani Morogoro, Fikiri Yusufu (37), jana aliibuka mshindi wa tatu wa sh milioni saba wa shindano la Voda Milionea.
Droo hiyo ya 21 ni sehemu ya promosheni ya miezi miwili inayowahusisha watumiaji wa mtandao wa Vodacom. Bahati Nasibu hiyo ilisimamiwa na ofisa kutoka Michezo ya Kubahatisha, Sadick Eliamsu.
Akizungumza mara baada ya droo hiyo juzi, Mratibu wa Mahusiano na Matukio wa Vodacom, Rukia Mtingwa, aliwataka wateja wa kampuni hiyo kuendelea kuongeza muda wa maongezi, ili kuweza kupata nafasi ya kujishindia zaidi.
Jumla ya washindi 21 wameshapatikana mpaka sasa tangu kuzinduliwa kwa promosheni hiyo.