UWEPO wa wakimbizi nchini si chanzo cha kuongezeka kwa vitendo vya uhalifu, vikiwamo vya ujambazi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Utetezi wa Haki za Binadamu mkoani Dodoma, Dk. Emmanuel Kandusi, alisema hayo alipokuwa akifungua semina ya waandishi wa habari iliyofanyika ijini Dar es Salaam jana.
Alisema hali hiyo imefanya hata haki ya wakimbizi isionekane na wakati mwingine wamewekwa katika kundi la watu waliokosa mwelekeo, hivyo kuhusishwa na matendo maovu kama ujambazi.
“Wakati wowote linaweza kutokea jambo fulani ukajikuta na wewe ni mkimbizi, haijalishi upo nchi ya amani,” alisema Dk. Kandusi.
Naye Mkuu wa Mradi wa Mtandao wa Asasi za Haki za Binadamu Kusini mwa Afrika kuhusu masuala ya wakimbizi na haki zao (SAHRINGON), Ancillah Nyanjige, alisema kuwa mkimbizi ana haki ya kupata maisha bora, chakula na malazi kama mtu mwingine yeyote.
Aliishauri jamii iwatambue wakimbizi na kuwatekelezea haki zao za msing