Kibondo
WANANCHI wa kada mbalimbali wilayani Kibondo, wameungana na wenzao kadhaa katika mikoa Mara, Mwanza na Kagera, kupinga maombi ya nchi za Rwanda na Burundi kupewa uanachama katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).
Wakizungumza na Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Diodorus Kamala jana, wananchi hao wamepinga wazi wazo lolote la kuzikaribisha nchi hizo katika EAC.
Moja ya sababu za kukataa kupokelewa kwa nchi za Rwanda na Burundi katika jumuiya hiyo ni pamoja machafuko ya kisiasa, ukabila na vita katika nchi hizo.
Aidha wananchi hao wameshauri Burundi na Rwanda wapewe masharti, ikiwa ni pamoja na kusalimisha silaha zilizozagaa mikononi mwa wananchi ambazo zimedaiwa kuhusika katika uharifu mwingi nchini.
Kwa upande wake jeshi la polisi wilayani Kibondo limeiomba serikali licha ya ushirikiano wa kijeshi na nchi za afrika mashariki Polisi nao wapewe fursa ya ushirikiano wa kipolisi na nchi hizo ili kupunguza uharifu unaofanyika mipakani.
Kamanda wa polisi wilaya ya Kibondo SSP Twaha Ramadhan amemwambia naibu waziri kuwa jeshi la polisi Tanzania limekuwa likifanya kazi kubwa na ngumu ya kuzuia uharifu katika mipaka bila kupata ushirikiano mkubwa toka kwa polisi wan chi jirani.
Dk. Kamala yuko katika ziara ya mikoa kadhaa akitangaza na kufafanua kazi za wizara hiyo ambayo ni mpya; kueleza fursa ambazo Watanzania wanaweza kuzipata kutoka EAC, na kukusanya maoni ya wananchi kuhusu Rwanda na Burundi kupewa uanachama EAC na muundo wa Shirikisho la Afrika Mashariki.
Oktoba 13, mwaka huu, Rais Jakaya Kikwete, atatangaza Kamati maalumu ya kukusanya maoni ya wananchi katika wilaya zote nchini kuhusu Rwanda na Burundi kupewa uanachama, na pia muundo wa Shirikisho