Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Michezo  »  Tanzania vs Mozambique
Tanzania vs Mozambique
By Marshy Abdu | Published  10/6/2006 | Michezo | Unrated
Tanzania vs Mozambique

Timu ya soka ya Taifa, Taifa Stars imeingia kambini kujiandaa na mechi yake ya pili dhidi ya kikosi cha Msumbiji.

Stars na Msumbiji wanatarajiwa kukutana kati ya Oktoba 6 na 8 huko Msumbiji katika mechi ya kundi la 12 ya kuwania kufuzu kucheza fainali za Mataifa ya Afrika.

Fainali hizo zitakafanyika Ghana mwaka 2008 na Tanzania chini ya kocha mpya, Marcio Maximo inatarajia kufanya kila linalowezekana ili kufika huko.

Ifuatayo ni orodha ya majina kamili ya wachezaji waliochaguliwa kwa ajili ya kujiandaa na mchezo huo ambao utafanyika ugenini.

MAKIPA: Juma Kaseja (Simba), Ivo Mapunda (Yanga) na Japhary Said (KMKM ya Zanzibar).

MABEKI:Dickson Daudi (Mtibwa), Mecky Maxime (Mtibwa), Nadir Haruob (Yanga), Said Morad (Ashanti), Haji Mbelwa (Rayon), Salum Swedi (Mtibwa), Shadrack Nsajigwa (Yanga) na Victor Costa (Simba).


VIUNGO: Renatus Njohole (Baulmes), Athuman Idd (Simba), Henry Joseph (Simba), Hussein Sued (Ashanti), Marleges Mwangwa (Kagera Sugar), Nizar Khalfan (Mtibwa) na Obadia Mungusa (Mwenge).

WASHAMBULIAJI: Bakari Kigodeko (Ashanti), Gaudence Mwaikimba (Yanga), Mussa Mgosi (Simba), Said Maulid (Yanga) na Emmanuel Gabriel (Simba).

Pia Maximo aliwataja wachezaji vijana ambao ni Godfrey Sharuti, Yassin Juma, Mecky Michael na Jerry Tegete.

Katika mechi ya kwanza, Stars iliibamiza Burkinafaso mabao 2-1 na hivyo kuifanya Tanzania kupanda nafasi 28 katika orodha ya Shirikisho la  Soka  Afrika (CAF)na nafasi ya 105 Duniani (FIFA) 

Kila la Kheri Tanzania, Kila la Kheri Taifa Stars.

Habri Tanzania.com inasema kwamba watanzania shangilia ushindi unakuja


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  3. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Nitaendelea kugombea nafasi za kisiasa- Balozi Karume
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Nthelezi Nesaa
  4. Linda Garner
  5. Marshy Abdu
  6. Prosper Kwigize
  7. Salehe Mmoro
  8. Ramadhan Semtawa
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.