Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Wafanyabiashara wafurika Makumbusho Waongezeka toka 66 hadi 450
Wafanyabiashara wafurika Makumbusho Waongezeka toka 66 hadi 450
By Habari Tanzania | Published  09/29/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Kuhamishiwa kwa kituo cha mabasi toka Mwenge kwenda Makumbusho katika Manispaa ya Kinondoni kumeongeza idadi ya wafanyabiashara wapya katika soko la Makumbusho lililokuwa likidoda kwa muda mrefu ambapo sasa wafanyabiashara kibao wanaendesha shughuli zao hapo.

Awali soko hilo lilikuwa na wafanyabiashara 66 pekee ambapo sasa, hadi kufikia jana, tayari idadi hiyo ilishapaa na kufikia wafanyabiashara 450.

Ongezeko hilo limekuja katika kipindi cha wiki sita kati ya nane zilizotangazwa na Manispaa ya Kinondoni kuwa zitatosha kukamilisha ujenzi wa kituo cha mabasi Mwenge.

Makamu Mwenyekiti wa soko la Makumbusho, Bw. Hassan Omary amesema kuwa ongezeko hilo linaweza kuwa changamoto mpya kwa Manispaa yao ya Kinondoni kuhakikisha kuwa kituo hicho hakihamishwi tena.

Alisema kati ya wafanyabiashara hao, 115 wapo nje ya soko kuzunguka stendi ya mabasi, 15 ni Mama Lishe na wote waliosalia wanauza bidhaa ndogondogo zikiwemo nyanya, matunda, mbogamboga na bidhaa nyinginezo zisizokauka katika soko lolote lile la maana kama lao.

Akasema Bw. Omary kuwa hivi sasa, ni meza chache zinazododa ambapo kati ya 220 walizo nazo na mabanda 70 yanayozunguka soko, tayari kuna wafanyabiashara kibao waliojitwalia nafasi na kuendelea na shughuli zao za kujiingizia vipato halali.

Hata hivyo, Bw.Omary akasema kuwa ongezeko hilo lingesaidia kuongeza pato la Manispaa kupitia kodi ya ushuru, lakini msimamo wa sasa wa serikali kutowatoza ushuru wafanyabiashara hao umekwamisha upatikanaji wa fedha hizo.

Hata hivyo, Bw. Omary alisema kuwa nafasi sokoni kwake hapo bado zipo bwerere na kusema kuwa kama utaratibu wa sasa wa kusisitiza uwepo wa matumizi ya kituo hicho cha mabasi, nafasi zote zingejaa.
  • SOURCE: Alasiri

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
This article has been added to your 'Articles to Read' list.
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.