UMOJA wa Makanisa ya Kikristo wilayani hapa, mkoani Mbeya, umetoa siku saba kwa wachungaji na maaskofu wanaojihusisha na vitendo vya ujambazi na dawa za kulevya kujisalimisha polisi kabla hawajaanza kutajwa.
Kauli hiyo imetolewa juzi na washiriki wa semina ya siku tatu iliyoandaliwa na umoja huo, waliosema kuwa wapo miongoni mwa wachungaji wanaojihusisha na vitendo viovu ukiwamo ujambazi wa kutumia silaha, uuzaji wa dawa za kulevya na kueneza virusi vya UKIMWI.
Wakinukuu aya ya Biblia, wamesema ni vema waanze kutoa vibanzi kwenye macho yao ndipo wataweza kutoa kwa wengine, hivyo wametoa siku saba za kujisalimisha, baada ya hapo wataanza kuwataja watuhumiwa kwa kupeleka taarifa zao kwa Mkuu wa Wilaya.
Akizungumza wakati wa ufungaji wa semina hiyo, Mwenyekiti wa umoja huo, Mchungaji Burton Msongole, alisema maazimio hayo yamefikiwa kutokana na kukithiri kwa vitendo hivyo ambavyo vinaiathiri jamii.
Alisema kuwa wameamua kuchukua hatua hiyo baada ya kukerwa na tabia ya baadhi ya wenzao ambao wanafahamika, ambao wanaitia doa kazi ya Mungu