Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Sheikh Yahya awageuka Waislamu
Sheikh Yahya awageuka Waislamu
By Habari Tanzania | Published  09/28/2006 | Habari za Kitaifa | Rating:
na Charles Mullinda

MTUMISHI wa Quran, Sheikh Yahya Hussein, amewageuzia kibao Waislamu, akisema kwamba wenyewe ndio walioamua kufutwa kwa Mahakama ya Kadhi.

Sheikh huyo ambaye pia ni mtaalamu wa nyota, aliwaambia waandishi wa habari katika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) jana kwamba, Waislamu walifanya hivyo kwa itikadi za dini.

Alisema Waislamu ndio walioishawishi serikali kupeleka muswada wa kufutwa kwa mahakama hiyo bungeni mwaka 1963 kupitia kwa aliyekuwa Waziri wa Sheria, Sheikh Amri Abeid Kaluta, aliyekuwa kiongozi wa Madhehebu ya Kadini.

Kauli hiyo ya Sheikh Yahya inakuja wakati kukiwa na mjadala mzito juu ya kurejeshwa kwa Mahakama ya Kadhi, kukiwa na makundi mawili, moja likipinga kwa kusema ni kinyume cha katiba na jingine likisema ni haki ya kidini ya Waislamu.

Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA), limeshaeleza msimamo wake wa kutaka kurejeshwa mahakama hiyo, wakati maaskofu kadhaa wameeleza kuipinga, wakisema italeta mpasuko nchini.

Wanasiasa nao wamegawanyika katika makundi mawili, baadhi wakishikilia kwamba lazima ianzishwe, kwa sababu ipo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Sheikh Yahya alikuwa amewaita waandishi wa habari, akisema alilenga kuzungumzia iwapo Mahakama ya Kadhi bado inahitajika au imepitwa na wakati, na kwa nini makanisa yalianzisha mahakama hizo, yakazisimamia na kuziendeleza hadi mwaka 1962 na jinsi Waislamu walivyoamua zifutwe bungeni.

“Ukadhi hapa nchini ulivunjwa na Waislamu wenyewe kwa itikadi za kidini. Waziri wa Sheria wa Tanganyika, hayati Sheikh Amri Abeid Kaluta, Mwislamu ambaye wakati huo alikuwa kiongozi mkuu wa Madhehebu ya Kadini, ndiye aliyeishawishi serikali kupeleka muswada bungeni kufuta Mahakama ya Kadhi.

“Muswada wa kufanya mabadiliko hayo uliokuwa ukiitwa ‘Magistrate Court Bill 1963, uliwasilishwa na kujadiliwa katika kikao cha tisa cha Bunge kilichofanyika Desemba 3 hadi 5, 1965.

“Muswada huu ulikuwa kimya na haukugusia chochote kuhusiana na Mahakama ya Kadhi au mahakama nyingine za aina hiyo, ili kuendelea kusimamia sheria za dini ya Kiislamu kwa kiwango mahsusi,” alisema Sheikh Yahya.

Alisema Wakristo wa madhehebu ya Kikatoliki, Kilutheri na Kianglikana, ndio walioanzisha na kuendeleza mahakama hiyo, kwa hoja zilizokuwapo wakati huo kuwa serikali ilikuwa za dini yao.

Aliwashangaa Wakristo kwa kuonyesha wasiwasi, baada ya kutaka kurejeshwa kwa Mahakama ya Kadhi wakati tangu utawala wa Wakristo wa Kireno, Wajerumani na Waingereza waliziendeleza mahakama hizo.

Alisema mahakama za Kislamu ziliundwa kwa tangazo la serikali namba 8 la 1925 lililotamka bayana kuwa masuala au mashauri yote ya ndoa, mirathi, talaka na mengine yanayohusika na Sheria za Kiislamu, yahukumiwe katika Mahakama ya Kadhi au liwali kwa kutegemea matakwa ya wahusika.

Mnajimu huyo, alisema Mahakama ya Kadhi inahitajika mara tatu zaidi kuliko ilivyokuwa wakati wa uhuru. Alisema umuhimu wa mahakama hiyo unatokana na kuanzishwa kwa vyama vingi vya siasa, ambako Waislamu waliogawanyika katika vyama hivyo laziwa wawe na kadhi wa kuwaunganisha.

Alitaja sababu nyingine ya umuhimu wa kuwapo mahakama hiyo, kuwa ni kuibuka kwa jumuiya nyingi za kidini baada ya BAKWATA, zinazodai ubora wa jumuiya zao na kupinga uongozi wa jumuiya nyingine.

Alisema sababu nyingine ni kwamba, misikiti kupewa usajili kamili wa udhamini na Wizara ya Sheria ambayo maimamu wao na wadhamini wanajitambua kuwa ni viongozi wa Waislamu.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments
  • Comment #1 (Posted by realbongolander)
    Rating
    Shehe kajichanganya...hajasema km sababu zilizowafanya waislam kuindoa hiyo mahakama ziemtafutiwa jibu au lah.
    Kingine alichoasahau huyu jamaa aliyepewa ulaji ni kuwa...kukubaliwa na wakwistu wa enzi zile za ukolononi hakumaanishi kuwa moja kwa moja na wakrsitu wa leo waikubali tuu..
    -waislam wansahahau kuwa kujinganganiza na serikali ni kutaka ifanya serikali ni ya kidini...wakati dini ni suala la mtu binafsi.Na ubinafsi huo ndio utakaomfanya mtu kuamua afuate vipi sheria za Mungu wkae km imani yake imtakavyo.
    -Pia sheikh kashindwa jua kuwa wakoloni walikubali an akuiweka kwa malengo yao ya kikoloni.Na wamissionary nao hawakuwa na ujanja zaidi ya kukubali.
    Nadhani imefika wakti waislam wanatakiwa wajue kuwa dini ni suala la mtu binafsi,na makubaliano na kundi la waniman wenzie,sheria za nchi ndio zitakuwa na final says...sasa wao kunganganiza imani yao ijadiliwe ktk vyombo vya umma,mambo yao yaamuliwe na umma,na watumie rasilimali za umma,km waendavyo hija...ni kukosa busara, kwani hata wapagani nao,au wasioamini kuwepo kwa Mungu,wakrsitu na wahindu wakidai hizo favour nchi itakuweje..?
    Kwanza shekh mwenyewe kasema kuwa waislam wamegawanyika sana...sasa k bakwata ambayo ilipaswa kuwa km chumbo kisicho na dhehebu ktk ya waislam kimeshindwa fanya kazi itakuweje,mahakama ya kadhi...ambayo itakuwa ikijulikana wazi kuwa nani wa dhehebu gani anayeshikilia kunono?Tayari waislam wenyewe kuna madhehebu waliyoyaona kuwa si waislam swafi...sijui ni vipi watatueleza kuwa majibu haya wanayo..?Wakristu wana mabarazara yao ya kisuluhishi,ila yote hayajangangania kupelekwa mpaka mungeni,sijui na nini...
    serikali kukubali haya ni kusema ile sera ya kutenganisha Kanisa na Serikali...ni ya kweli kwa wote na si kwa msikiti na serikali...basi km katatizo ni maneno...tutafute mengine..km kutenganisha dini na serikali...pengine waislam wataelewa,wanawez kuwa wakifurahi kusikia kanisa na serikali.
    Sasa km zanzibar wamefikia kuingiliz uhuru binafsi,na kufikisha watu mahakamani kwa kula na kuuza chakula hadharani basi ipo taabu...hapa kuna majibu.
    Waamini wa kiislam inabidi wajifunze ienzi dini yao ndani ya mioyo yao na si kutaka kila mtu ajitume kuwatunzia kilicho mali kwao....wao ndio wajifuatie sheria zao,km wengine wafuatavyo ila zikipingana za serikali basi wembe wa sheria ya nchi ushike njia yake.CCM walishakula kura zenu...kwa hadi mbuzi hii.ila haina dili

     
Submit Comment


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.