Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Ramadhan Semtawa  »  Waziri asema ndege za serikali Tanzania zimezeeka
Waziri asema ndege za serikali Tanzania zimezeeka
By Ramadhan Semtawa | Published  09/27/2006 | Ramadhan Semtawa | Unrated

Na Ramadhan Semtawa
WAZIRI wa Miundombinu, Basil Mramba, amesema karibu ndege zote za serikali zimezeeka na zinapaswa kununuliwa nyingine mpya.

Akizungumza na gazeti hili ofisini kwake hili jijini Dar es Salaam jana, Mramba alisema kama ni kuzingatia sheria za kimataifa za usafiri wa anga, ndege hizo za serikali zisingeruhusiwa kuruka angani.

Mramba alisema sababu zinazofanya kuwepo haja ya kununua ndege hizo, ambazo ziko kwa Wakala wa Ndege za Serikali ni pamoja na kwamba ndege hizo aina ya Fokker zina zaidi ya miaka ya 30 tangu ziliponunuliwa, hivyo ni hatari kwa usalama wa abiria na kuongezeka gharama uendeshaji kutokana na kuzeeka.

Hata hivyo, waziri Mramba alisema katika mwaka huu wa fedha, serikali haijatenga bajeti kwa ajili ya kununua ndege nyingine mpya, kwani bado yanaangaliwa maeneo mengine ya kipaumbele.

Mramba alizitaja ndege hizo ambazo zinamilikiwa na serikali kupitia wakala wake, kuwa ni Fokker 50 na Fokker 28 Jet na nyingine ndogo ambayo alisema hata hivyo, haitumiki sana.

"Ndege za serikali zimezeeka, kama ni sheria, basi ndege zilizozidi miaka 30 katika nchi nyingine haziruhusiwi kuruka angani," alisisitiza Mramba.

Hata hivyo, Mramba alikiri kwamba gharama za kununua ndege moja ni kubwa ambapo huanzia wastani wa dola za Marekani 25 hadi 40 milioni.

Kuhusu taarifa kwamba, kuna kampuni ya ndege kutoka Brazil ambayo iko nchini kutaka kuiuzia serikali ndege, alisema hakuna mazungumzo yoyote ambayo yamekwishafanyika kati ya serikali na kampuni hiyo.

Mramba alisema anafahamu kwa kusikia, kwamba kuna kampuni hiyo ambayo iko nchini na kuongeza kuwa, kama itahitaji mazungumzo na serikali haitakuwa tatizo


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
This article has been added to your 'Favourites' list.
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.