Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Bodi ya Wahandisi kujadili kuporomoka kwa ghorofa Dar
Bodi ya Wahandisi kujadili kuporomoka kwa ghorofa Dar
By Habari Tanzania | Published  05/25/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated

Na Epson Luhwago

BODI ya Usajili wa Wahandisi nchini (ERB) kwa kushirikiana na Chama cha Wahandisi Washauri Tanzania (ACET), imeandaa mkutano wa siku moja kujadili pamoja na mambo mengine kuporomoka kwa jengo la ghorofa tano la Chang'ombe, Dar es Salaam.

Kaimu Msajili wa ERB, Injinia Steven Mlote, aliwaambia waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam kuwa k atika mkutano huo utakaofanyika kwenye hoteli ya Kunduchi Beach and Resort, Dar es Salaam pia Bodi itatoa taarifa ya juu ya mambo iliyoyaona wakati wa

ukaguzi wa majengo mbalimbali nchini.

"Bodi kwa kushirikiana na ACET tumeona ni vyemakuandaa mkutano huu ili kukumbushana mambo mbalimbalikutokana na hali ilivyo sasa katika shughuli zakihandisi na matukio ya hivi karibuni," alisema.

Injinia Mlote alisema hatua hiyo pia imechukuliwa ilikuwakumbusha wahandisi na wadau wa ujenzi juu yataaluma na kazi za kihandisi kwa maendeleo ya taifa.

Alisema katika mkutano huo utakaohusisha wahandisiwashauri, madhumuni hasa ya mkutano huo wa mashauriano ni kuweka mtandao baina ya wahandisi washauri ilikuwasaidia kubadilishana ujuzi na uzoefu katika kazi zao.

Kaimu Msajili alisema nia hasa juu ya hilo nikuimarisha kazi ya ushauri wa kihandisi na usimamiziwa ujenzi katika shughuli za ujenzi kwenye maeneombalimbali nchini.

"Lengo la mkutano huu pia ni kuwakumbusha wahandisiwashauri juu ya vigezo vinavyotakiwa katika shughulizao kwa mujibu wa Sheria ya Usajili wa Wahandisi, taratibu, miiko na maadili ya wahandisi," aliongeza.

Mlote alisema hivi karibuni kumejitokeza matukioyasiyofuata taratibu, sheria na maadili ya taaluma yauhandisi miongoni mwa wahandisi na wahandisi washauri,hivyo kusababisha hadhira mbaya kwa jamii juu yamwenendo mzima wa taaluma ya kihandisi.

Katika mkutano huo, kwa mujibu wa Mlote, wahandisiwashauri wataelezwa taarifa juu ya vitendo vinavyokwenda kinyume na maadili ya kazi vinavyofanywa na baadhi ya wahandisi washauri.

Injinia Mlote alisema mkutano huo wa aina yake katikataaluma na fani ya uhandisi, pia utahudhuriwa na wahandisi wataalam wa muda mrefu hapa nchini.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.