Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Jengo la NEC Z’bar lauzwa
Jengo la NEC Z’bar lauzwa
By Habari Tanzania | Published  09/25/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar

JENGO lililokuwa likitumika kama Ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Zanzibar, limeuzwa kinyemela na kugeuzwa ghala la kuhifadhia saruji.

Jengo hilo lililopo Mtaa wa Kwa Abass Hussein mjini Zanzibar, limeuzwa hivi karibuni na sasa linatumika kwa shughuli za kibiashara. Askari waliokuwa wakilinda ofisi hizo, wameondoka.

Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), ambayo ni wakala wa NEC, Masauni Yussuf Masauni, alithibitisha kuwapo kwa taarifa za kuuzwa kwa jengo hilo.

“Hata sisi tunasikia taarifa hizo, lakini Tume ya Taifa ya Uchaguzi inaweza kuzungumzia vizuri suala hilo, kwa vile sisi tunavyofahamu jengo hilo walipewa Tume ya Taifa kuendeshea shughuli zao za uchaguzi,” alisema.

Uchunguzi wa Tanzania Daima umebaini kuwa jengo hilo limechukuliwa na kigogo mmoja serikalini (jina linahifadhiwa) ambaye ana historia ndefu na siasa za visiwani.

Habari zilizopatikana zimeeleza kwamba Diwani wa eneo hilo, Khamis Amour, amejitahidi kufuatilia sakata hilo, ikiwa ni pamoja na kukutana na Kaimu Mkurugenzi wa ZEC, Idrisa Jecha.

Hata hivyo, imeelezwa kwamba ofisa huyo naye alishangazwa na hatua hiyo kwa vile alidai ofisi yao haina taarifa yoyote kuhusu ukarabati wa ofisi hiyo unaoendelea pamoja na kugeuzwa ghala la saruji.

Makamu Mwenyekiti wa NEC, Omar Makungu, alipoulizwa na Tanzania Daima, alisema kwamba wao wanafahamu kuwa jengo hilo hadi sasa ni lao kwa vile walipewa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

“Sisi tunafahamu jengo hili bado ni letu na hatuna taarifa yoyote kama limeuzwa, na ofisi zetu bado zitaendelea kuwapo hapo hapo,” alisema Makungu, ambaye pia ni Naibu Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar.

Mratibu wa ZEC, Salum Juma Mgunya, alisema hana taarifa ya kuuzwa jengo hilo, ingawa ameshuhudia likifanyiwa matengenezo makubwa.

Jengo hilo zamani lilikuwa likimilikiwa na Shirika la Biashara na Viwanda, kama kituo cha ushirika wa viwanda vidogo vidogo, ambalo lilishindwa kujiendesha kibiashara.

Katika siku za hivi karibuni kumekuwapo na wimbi kubwa la majengo ya Serikali ya Zanzibar kuchukuliwa na baadhi ya wakubwa au familia za wakubwa bila ya kutangazwa zabuni.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.