Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Wapagazi Mlima Meru wahitaji kuelimishwa utalii
Wapagazi Mlima Meru wahitaji kuelimishwa utalii
By Habari Tanzania | Published  09/24/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Na Mussa Juma, Arusha
HIFADHI ya Taifa ya Arusha (ANAPA), imekitaka Chama cha Wapagazi wa Mlima Meru kuwaelimisha wanachama wake kutoa huduma bora kwa wageni wanaopanda mlima huo, vinginevyo watazuiwa kutoa huduma hiyo.

Mhifadhi Mkuu wa hifadhi hiyo, Erastus Lufungilo alitoa wito huo juzi wakati akizungumzia malalamiko ya wamiliki wa kampuni za utalii kuwa baadhi ya wapagazi wamekuwa wakitoa huduma mbaya kwa watalii na hivyo wanalazimika kuja na wapagazi kutoka mjini Arusha au Moshi.

Alisema kutokana na malalamiko ya mara kwa mara kuhusu wapagazi, hifadhi hiyo inakusudia kutoa mapendekezo kwa Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (TANAPA) kuruhusu wapagaji wengi ambao hawatoki katika chama hicho kutoa huduma.

"Mwelekeo wetu wa baadaye ni kufanya shughuli za upagazi kuwa sawa kama ilivyo katika hifadhi ya Mlima Kilimanjaro,lakini makampuni ya utalii yakianza kuleta wapagazi tuna imani idadi kubwa itatoka kwa wapagazi wanaoishi jirani na mlima huu,"alisema.

Alisema ANAPA itaendelea kukisaidia chama cha wapagazi wa Mlima Meru katika kutoa elimu kwa wanachama wake ili waboreshe huduma zao kwa wageni na hatimaye kuingia katika ushindani.

Naye, Mwenyekiti wa chama hicho cha wapagazi hao wa Mlima Meru,Tutason Ako akizungumzia malalamiko hayo, alisema ni kweli yamekuwa yakitolewa, lakini wao kama viongozi pia wamekuwa wakitoa elimu kwa wanachama wao.

"Sisi kama chama tunajitahidi, wanachama wetu watoe huduma bora, lakini kama kuna matatizo ni madogo madogo ambayo tunaimani yatakwisha,"alisema Ako.

Mawakala wa watalii na wamiliki wa makampuni ya utalii wamekuwa kwa muda mrefu wakilalamikia wapagazi wa kutoka eneo linalozunguka mlima huo kuwa wamekuwa wakifanyakazi chini ya kiwango na hivyo kuathiri utalii wa kupanda mlima huo.

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.