Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Mtoto afariki akisaka fedha za sherehe
Mtoto afariki akisaka fedha za sherehe
By Habari Tanzania | Published  09/22/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Na Lilian Lugakingira, Bukoba

MTOTO Blavias Godpride (14), mkazi wa Kyasha, Kata ya Buhembe katika Manispaa ya Bukoba, amefariki dunia baada ya kufukiwa na kifusi wakati akichimba mchanga wa kuuza ili apate fedha za kufanyia sherehe.

Mtoto huyo ambaye amemaliza darasa la saba mwaka huu katika Shule ya Msingi Nyakato, iliyoko katika manispaa hiyo, alikwenda kuchimba mchanga katika eneo la Kashekulo kwa ajili ya kuuza.

Imedaiwa kuwa kutokana na uwezo mdogo wa wazazi wake, alishindwa kupata fedha za kujumuika na wenzake kujipongeza baada ya kumaliza mtihani wa taifa wa darasa la saba, uliomalizika Septemba 14, mwaka huu, aliamua kuanza shughuli za kuchimba mchanga wa kuuza ili apate fedha za sherehe hiyo.

Wakati mtoto huyo akichimba mchanga pamoja na wenzake, udongo uliporomoka na kumfukia na shughuli za kumwokoa zilifanyika, lakini alipotolewa katika kifusi hicho, alikuwa amekwisha fariki.

Mwili wa mtoto huyo ulichukuliwa na ndugu na jamaa kwa ajili ya mazishi na Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Adihaki Rashid, alithibitisha kuwepo kwa tukio hilo.

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.