Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Zanzibar kuajiri walimu 3,000 wa sekondari
Zanzibar kuajiri walimu 3,000 wa sekondari
By Habari Tanzania | Published  09/22/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Na Mussa Haji Foum, Zanzibar

SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar ataajiri walimu wapatao 3,000 wenye shahada na stashahada, kwa ajili ya shule za sekondari, katika kipindi cha miaka mitano ijayo, ili kuinua kiwango cha elimu nchini.

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali, Haroun Ali Suleiman, alisema katika kipindi hicho, walimu 1,200 wenye shahada na1,500 wenye stashahada, wataajiriwa ili kuondoa tatizo la walimu visiwani humo na hasa walimu wa masomo ya sayansi.

Alisema serikali inaendelea na jitihada zake za kuwaelimisha wananfunzi katika vyuo vikuu viliopo Zanzibar, ikiwa pamoja Chuo Kikuu cha Ualimu cha Chukwani na Chuo Kikuu cha Zanzibar kilichopo Tunguu.

Waziri Haroun alisema katika kipindi hicho, serikali inakusudia kujenga shule kumi za secondari za kisasa, zitakazoanzia na kidato cha kwanza hadi cha sita.

Alisema shule hizo zitakuwa na maabara za kisasa, vyumba vya komputa, viwanja vya michezo kwa wanafunzi wanawake na wanaume.

Aliongeza kuwa hatu hiyo, itawawezesha wanafunzi watakaofaulu kuingia kidatu cha tano kujiunga na shule hizo na kuondokana na usumbufu wa kufuata masomo mijini.

Alifahamisha kuwa vyuo vya elimu mbadala, vitajengwa katika maeneo ya Mkokotoni Unguja na Vitongoji kisiwani Pemba, ili kutoa fursa kwa wanafunzi waliokosa kuendelea na masomo kutokana na sababu mbali mbali.

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.