Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Filamu ya Watumwa wa vito haitavuruga soko la tanzanite
Filamu ya Watumwa wa vito haitavuruga soko la tanzanite
By Habari Tanzania | Published  09/21/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Na Mussa Juma, Arusha

KAMPUNI ya Wawekezaji ya Tanzanite One, imesema filamu ya watumwa wa vito ambayo inaonyesha utumikishwaji watoto katika madini ya Tanzanite Mererani, haitavuruga bei ya madini hayo.

Rais wa kampuni hiyo ambayo inajihusisha na uchimbaji wa madini ya tanzanite Mererani, Ian Harebottle, alisema kuwa ingawa filamu hiyo ina madhara katika soko la madini hayo, lakini kwa kuwa tanzanite inatoka Tanzania pekee, itakuwa ni vigumu kuvuruga bei.

"Bado thamani ya madini haya ipo juu, hivyo kuiporomosha kwa haraka katika soko la madini hayo kimataifa si rahisi kwani pia tayari tumetangaza sana madini haya, " alisema Harebottle.

Aliongeza kusema kuwa ,waandaaji wa filamu hiyo pia walifika katika eneo lao la kitalu C katika machimbo hayo lakini hawakuwapa ushirikiano wa kutosha kutokana na kutojua lengo hasa la filamu hiyo.

"Walikuja kwetu hatukuwapa ushirikiano kwani tulihisi hawakuwana lengo zuri," alisema.

Hata hivyo, alisema kampuni yake kupitia taasisi yake ya Tanzanite Foundation imekuwa na mikakati mingine ya kutangaza madini hayo nje ya nchi.

Harebottle alisema hivi sasa nchi mbali mbali duniani zimekuwa zikinunua madini hayo kwa ajili ya kutengeneza vito na kwa shughuli nyingine tofauti na miaka ya nyuma.

Filamu la Utumwa wa vito ambayo inaonesha utumikishwaji watoto katika migodi ya madini ya Tanzanite Mererani iliyoandaliwa na Shirika la Habari la Kimataifa lilisilo la kiserikali la IRIN imezinduliwa hivi karibuni nchini Marekani


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.