Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Z’bar yatangaza bei ya vyakula
Z’bar yatangaza bei ya vyakula
By Habari Tanzania | Published  09/19/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar

SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza viwango vipya vya bei za vyakula ili kukabiliana na mfumko wa bei.

Uamuzi huo umetangazwa jana na Waziri wa Biashara, Utalii na Uwekezaji, Samia Suluhu Hassan, kutokana na kikao cha serikali na wenye kampuni za uingizaji vyakula Zanzibar.

Waziri Samia alisema kwamba kuanzia sasa ni marufuku kwa wafanyabiashara wa mchele, unga wa ngano na sukari kuuza bidhaa hizo bila kuzingatia viwango vya bei vya serikali.

Alisema kwamba wanachukua uamuzi huo baada ya kuafikiana na wafanyabiashara hao, kwamba kodi ya forodha itapunguzwa kwa asilimia 25, ili nao waweze kuwauzia wananchi kwa unafuu.

“Kuanzia sasa, mchele utauzwa kilo moja sh 600, badala ya sh 700, sukari sh 1,050 badala ya sh 1,000, unga wa ngano sh 600 badala ya sh 700,” alisema Waziri Samia.

Alisema kwamba mchele wenye chenga nyingi utauzwa sh 500, lakini hakusema mchele wa Mbeya wala ule mwembamba kutoka India (Basmat) utauzwa kwa sh ngapi.

“Watakaokwenda kinyume na viwango hivi vya bei, watakamatwa na kufikishwa mahakamani,” alisemaWaziri Samia.

Alieleza kwamba Waziri wa Biashara amepewa mamlaka, kwa mujibu wa sheria namba 2 ya 1995, kupanga viwango vya bei kulingana na mwenendo wa soko la dunia.

Alisema kwamba, katika kikao hicho wafanyabiashara wamekubali kupunguza viwango vya faida kwa asilimia 10, kutokana na serikali kuwapatia msamaha wa kodi ya asilimia 25 kwa bidhaa hizo za vyakula.

Hii ni mara ya kwanza serikali kutangaza viwango vya bei za bidhaa za vyakula, tangu kuruhusu mfumo wa soko huria la biashara.

Waziri Samia, alisema viwango hivyo vya bei vitakuwa vikipitiwa kila baada ya miezi miwili, ili kuangalia mabadiliko ya soko la dunia na gharama za ununuaji na usafirishaji.

Katika mkutano wake na waandishi wa habari, Mwenyekti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara, Wenye Viwanda na Wakulima, Abdallah Abbas, alisema hatua hiyo itawasaidia wafanyabiashara wa Zanzibar na wananchi.

Hata hivyo, alisema uchakavu wa Bandari ya Zanzibar umekuwa ukisababisha kero kwa wafanyabiashara, kwa vile mizigo mingi huchelewa kutolewa na hivyo kusababisha gharama kuongezeka.

Mwenyekiti huyo alisema kitendo cha serikali kukaa na wafanyabiashara na kuwapunguzia kodi kwa asilimia 25 katika kipindi hiki cha mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan, kitaleta unafuu wa upatikanaji bidhaa kwa wananchi, wakiwamo wale wa vijijini.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.