Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Kawawa awaasa wakulima Namtumbo
Kawawa awaasa wakulima Namtumbo
By Habari Tanzania | Published  09/18/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Na Albano Midelo, Ruvuma

MBUNGE wa Namtumbo, Vita Kawawa, ametoa rai kwa wakulima nchini kuuza mazao yao kwa kutumia vipimo mizani badala ya kutumia vipimo visivyo halali.

Kawawa alisema wakulima wakitumia vipimo halali, watapata faida badala ya kuendelea kunyonywa kwa kuuza mazao kwa walanguzi kwa kutumia kipimo cha ‘dumla’.

Alisema hayo hivi karibunii wakati wa majumuisho ya ziara ya kulitembelea jimbo hilo katika Kata ya Namtumbo kwa lengo la kuwashukuru wapiga kura.

“Acheni kuuza mazao yenu kiholela, mkubaliane kuuza mazao kwa pamoja ili mpate bei nzuri, tena mpime kwa mizani ili walanguzi wasiendelee kuwanyonya, vinginevyo mtaendelea kunyonywa,” alisema Kawawa.

Akizungumzia zao la tumbaku, mbunge huyo aliwataka viongozi wa vyama vya ushirika kuangalia mikataba wanayowekeana na kampuni za tumbaku, na iwapo mkataba haueleweki, wawaombe wanasheria wa serikali na halmashauri ili mikataba hiyo iwe na manufaa kwa wakulima.

Kuhusu usambazaji wa mbolea ya ruzuku katika maeneo ya vijijini katika msimu

uliopita, Kawawa alisema baadhi ya mawakala hawakuwa waaminifu baada ya kupata kibali cha kusambaza mbolea, waliuza kwa bei ya ulanguzi na kupeleka mifuko michache ya mbolea katika maeneo waliyopangiwa.

Alitoa wito kwa viongozi wa vijiji katika msimu huu wa kilimo, kuhakikisha mawakala wanafikisha kiasi chote cha mbolea walichopangiwa kulingana na kibali walichopewa ili wakulima wasiendelee kuuziwa mbolea ya ruzuku kwa bei kubwa.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.