Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Nthelezi Nesaa  »  Maskini Papa Bendicto XVI!
Maskini Papa Bendicto XVI!
By Nthelezi Nesaa | Published  09/17/2006 | Nthelezi Nesaa | Rating:
Na Mwandishi wa HabariTanzania.com, Canada
Tarehe 15 Septemba dunia ilizizima hasa ile ya kiislamu. Ilizizima kwa hasira na jazba baada ya kiongozi wa kanisa la kikatoliki la Roma, Papa Bendikto wa kumi na sita, kunukuu maneno ya mtawala kwa kikiristo wa karne ya nne. Mtawala yule alisema nionyeshe jpya aliloleta Mohamad zaidi ya mauaji, ukatili na kueneza dini kwa upanga.
 
 Papa alinukuu maneno hayo alipokuwa ziarani nchini mwake wiki moja kabla ya sakata hili. Alikuwa akitoa mhadhara kwenye chuo kikuu kimoja nchini humo.
 
 Kimsingi Papa hakuwa na nia mbaya ingawa maneno yake yalichukuliwa vibaya kama alivyoomba msamaha siku iliyofuata.
 Alichosahau Papa ni kwamba hata yeye nyumba yake si salama linapokuja suala la ni dini gani ilienezwa kwa ukatili na mauji.
 Uislam na ukristo kadhali vilienezwa kwa mauaji,vita,unyonyaji hata udhalilishaji.
 
 Hivyo basi hata hao waislamu walioudhiwa na kauli iliyonukuliwa inabidi kwanza waelewe kuwa hawawezi kuandika upya historia na pili wajue wazi kuwa pamoja na dini kuhubiri upendo na mengineyo,dunia inajua kuwa chimbuko la dini zote za kimamboleo ni baya tu.
 
 Wale wanaokumbuka kwa mfano madhara ya utumwa,watakubaliana nasi kuwa walioendesha biashara hii haramu ni waarabu na wazungu.
 
 Pia wakirejea vita kama vile Badr utekaji wa ulaya uliofanya na Othman, wataficha nyuso zao kwa aibu kama kweli chanzo cha maandamano yaliyoshuhudiwa huko India,Pakstani,Palestina ambako tunaambiwa makanisa mawili yalishambuliwa kwa risasa, Iran na kwingineko.
 
 Nani asiyejua kuwa baadhi ya amri kama vile kupiga watu mawe,kuwakata mikono,kuwatenga wanawake, kuwaua murtadi n.k ni ukatili tu?
 
 Kimsingi kwa mfano ukichukua viwango na tafsiri za haki za binadamu za dunia ya sasa,mafundisho yote ya torati ya Musa ni ukatili na unyama usio na ulazima wala yasiyofaa kwa wakati huu. Ni mambo yaliyopitwa na wakati ambayo yalilenga kuwastaarabisha walawi.
 
 Sasa hebu tuangalie Papa amesimama wapi kuhusiana na historia ya kanisa lake. Kuna uwezekano kuwa Papa bila kujua alijikuta kwenye kile waswahili husema nyani haoni nonihino lake.
 
 Kwanza nani asiyejua kuwa mzizi na chanzo cha ukiristo ni umwagaji damu ulioanzia Golgota. Nani hashangai jinsi wakristo wanavyoendelea kutumikishwa chini ya ushirikina wa kisasa ambao hadi tunaandika dunia imeufumbia macho. Hivi nani aweza kula nyama ya mpendwa wake na kumalizia kwa damu yake hata kama ni kwa mfano?
 
 Hili lingefanywa na dini za kiafrika lingeandikwa dunaia nzima na kusema waswahili wanakula nyama za watu yaani cannibalism.
 
 Tutatoa historia kidogo tu ya karne ya kumi na moja juu ya mauaji yaliyofanywa na kanisa la Roma analoliongoza Papa Bendikto.
 
 Mnamo mwaka 1252, Papa Innocent IV alitoa tamko la kipapa lililojulikana kama Ad exstipada. Tamko hili lilielekeza manyanga au na mawakala wa kanisa kuwaua wapinzani wa wakati huo yaani waprotestanti ambao liliwaita heretics. Katika kutekeleza tamko hili la kiuaji mauji makubwa kwa njia za kinyama zaidi yalifanyika. Maana watu walichomwa moto,kuvuliwa nguo,kungolewa macho na mengine kama hayo.
 
 Hiyo haikutosha. Kwani mwaka Ad exstripada iliendelea kupewa baraka na mapapa waliofuata baada ya Papa Innocent.
 Alexander IV (1254-61; Clemence IV (1265-68); Nicholaus IV (1288-92) Bonephace VIII (1294-1303) na wengine waliendelea kukazania kutumika kwa tamko hili chafu la kipapa.
 
 Katika ngwe ya pili ya mauaji haya watu walikatwa nyayo, walichomwa kwa vyuma vya moto sehemu nyeti za mwili,kunwagiwa maji ya baridi na njia nyingine za kinyama na utesaji mkubwa ambao binadamu hakuwahi kuushuhudia.
 
 Katika unyama huu historia inasema kuna vitu vilivyotumika kama Iron virgin na Spanish boots haviwezi kusahaulika.
 
 Kwa wale watakaotaka rejea tunawashauri wasome, Redpath’s history of the world. Hebu turejee kutoa baadhi ya visa vya mauaji yaliyofanywa na kanisa vilivyoitingisha historia ya mwanadamu.
 
 Francis Gamba (1554) alipopinga mauaji yaliyondeshwa na kanisa alilazimishwa kutubu na kufuta maneno yake. Alipokataa alinyofolewa ulimi maskini. Waliokuwa na mawazo kama yake walichomwa kwa kumwagia chuma cha moto, molten kwenye matundu ya macho na masikio. Papa inabidi ajitahidi kusoma historia ili asijikwae bure hata kama nia yake siyo kuwashutumu wenzake.
 
 Mwaka 1209 mji wa Beziers ulivamiwa na mawakala wa Papa ambapo watu wapatao 60,000 waliuawa kinyama.
 Hii haikutosha.
 
 Mwaka 1211 Gavana wa Lavaur alinyongwa huku mkewe akifungiwa jiwe na kuzamishwa kwa kosa la kupingana na amri ya kanisa ya kuwaua wapinzani wapatao 100,000. Hawa walijulikana kama Albigenses au waprotestanti.
 
 Mwaka 1562 chini ya amri ya Papa Pius IV mauaji maarufu ya Orange yalifanyika ambapo wahanga walichinjwa na kudhalilishwa vibaya sana.
 
 Mwaka 1572 Huguenots au waprotestanti kama walivyojulikana kipindi hiki waliuawa.
 Baada ya mauaji haya yalifuatia mauaji ya Paris ambapo Papa Grigory XIII aliadhimisha misa ya kumshukuru Mungu kwa mauaji haya kwenye kanisa la Mt. Barthromeo.
 
 Kwa furaha ya ukumbusho wa matukio hayo ya Orange na Paris ilitengenezwa sarafu iliyobeba picha ya Malaika akiwa ameshika panga mkono mmoja kuwamaliza wapinzani na msalaba mkono wa pili kuuimarisha ukristo.
 Sarafu hiyo ilibeba maneno "ugonottorum stranges 1572.
 
 Kwa uchache huo ndiyo ushahidi wa kuonyesha kuwa nyumba ya papa siyo safi. Tunaamini kuwa alilijua hili. Kama lengo la Papa kama ilivyokuwa azma yake ya mwanzo ni kuleta usuluhisho wa kiimani, hakufanya kosa kurejea historia maana siku zote kusuluhisha ni kama kufanya kesi mahakamani ambapo matukio hurejerewa.
 
 Kwa bahati mbaya waislam kwa vile wameishajenga dhana kuwa dunia haiwapendi hasa baada ya dini hii kuhusishwa na ugaidi, walielewa ndiyo siyo.
 
 Pia kuna haja ya dunia kuanza kutafuta jinsi ya kushughulikia tabia mbaya inayoanza kujitokeza ambapo watu chini ya kisingizio cha dini yao wanataka wasisemwe wala kuambiwa ukweli.
 
 Tabia hii bila shaka ndiyo mama wa uhafidhina unaoisumbua dunia iwe ni kutoka kwa waislamu au wakristo.
 
 Kimsingi somo tunalolipata ni utukufu wa dini zetu za kiasili ambazo hazina historia ya uchafu,uongo,udhalilishaji wala mauji kama dini hizi mbili za kikoloni ambazo zimeanza kuwa kero na tishio la usalama wa wale tusioziamini.
 
 Bahati mbaya dini hizi zimeanza kujijengea uhalali kiasi cha kutishia mstakabali mzima wa dunia.
 
 Kimsingi kilichosemwa na Papa hakikuwa kipya wala kibaya bali kurejea historia. Kama kungekuwa na nia mbaya basi Papa angekuwa sawa na kasa anayemcheka kobe au ng’ombe anayemcheka nyati. Kwani dini zote zina damu na dhambi nyingi mikononi mwake.

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments
  • Comment #1 (Posted by Latorino)
    Rating
    Nzuri sana na endelea kutuletea mambo mazuri kama haya. Nilikuwa sijui kama Kanisa lilishawahi kufanya unyama kama huo uliouelezea.
    Bwana akubariki
     
  • Comment #2 (Posted by Jackson Mabiti)
    Rating
    Kweli nyani haoni ....lake nimeamini.Mwandishi ametusaidia kujua kuwa kumbe kati ya waislam na wakristo hakuna aliye salama.
    Ama kweli wakoloni walituweza. Wakiudhiana wanatukimbilia sisi ili tumalizane.
    Hongera Papa kwa kutekenya donda.
    Jack Mabby
     
  • Comment #3 (Posted by kwiza)
    Rating
    Ebwana nimekukubali wewe ni mkali na ni mtaalam wa uchambuzi mungu akuzidishie hiyo fani uliyokuwa nayo
     
  • Comment #4 (Posted by Stephen Kibusi)
    Rating
    Excellent job.

    Well analyzed and articulated points.

    I liked the respect you gave on our holy holy and peaceful traditional spiritual rituals. We lost a great deal of who we are and sometimes i wonder if through christianity and/or Islam, we are not just worshiping the wrong Gods. We forsaken our true God or we are worshing the same one but in a wrong way. We pray so much in African, see what we end up getting!!!!!.....they dont do as much as we do but look at them ....blessed, the more they sin the more they develop, the more they curse God, the more he/she blesses them. I think something is missing Africa!!!!!.

    What touches me the most, is we are too fanatical to these two foreign religions, we forget that being Tanzanian...being African... should come first before these religions. Why kill each other because Islam, why kill one another because of Christianity. Shame on you Africa!!!!!!

    Great job man, keep it up.

    Kibusi
    6499 Waegwoltic Ave,
    Halifax, Nova Scotia,
    B3H 2B5, Canada.
     
  • Comment #5 (Posted by Adelard)
    Rating
    Ooh! Imetulia sina chakuongeza walakusema endelea kutufungua macho
     
  • Comment #6 (Posted by mwambata kiambata)
    Rating
    Umechambua vizuri na kwa makini. ILa mwenye imani haba akisoma kichwa kichwa, kwa yule aaminiye iwe kwa mkristu au mwuislam, kunauwezekano wa kupoteza imani yake. Hongera kwa kumtetea vizuri Papa Benedikto XVI.
     
  • Comment #7 (Posted by mwambata kiambata)
    Rating
    Why killing each other because of religion? We are have the same origin regardless of beliefs o colors. Shame to all the citizens of the world, not only on you Africa, as pointed above Stephen Kibusi!!!
     
Submit Comment


Article Options
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  3. Is Tanzania a safe place to invest?
  4. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
  5. Nitaendelea kugombea nafasi za kisiasa- Balozi Karume
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Linda Garner
  4. Nthelezi Nesaa
  5. Marshy Abdu
  6. Prosper Kwigize
  7. Salehe Mmoro
  8. Ramadhan Semtawa
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.